JACK MAISHA PLUS, RUBI WAFANYA MAZOEZI KUONDOA ‘VITAMBI’


MSHIRIKI wa Shindano la Maisha Plus Season II, Jacqueline Dastan ‘Jack Maisha Plus’ na shosti wake ambaye ni bosi wa Kundi la Nderemo Arts Group, Khadija Kasongo ‘Rubi’ wameanza kufanya mazoezi ya viungo kwa lengo la kuondoa ‘vitambi’.
Wasanii hao wameamua kuingia kwenye ‘tizi’ baada ya kuona vitambi vinakuwa tishio kwao, jambo ambalo limekuwa likiwakosesha raha kwani wanahisi hawana mwonekano mzuri.


Jacqueline Dastan ‘Jack Maisha Plus’.

“Tunafanya mazoezi asubuhi na jioni, lazima matumbo yapungue, si unaona kama yameanza kupungua kidogo?” alisema Rubi ambaye siku za karibuni aliwahi kuzichapa kavukavu na Jack kwa sababu ya kudaiana licha ya kuwa ni marafiki wakubwa.
Pamoja na mazoezi hayo ya viungo, Rubi alisema pia wanakunywa maji ya moto kila siku asubuhi ili kuyeyusha mafuta mwilini na wanapunguza vyakula vyenye mafuta mengi. 

 
“Usiku mara nyingi tunakula matunda tu badala ya chipsi kuku kama zamani. Unajua mwanamke ukiwa na tumbo kubwa kwa kweli haupendezi kabisa,” alisema Rubi.
Aliongeza kuwa ‘wachumba’ wengi siku hizi hawapendi wanawake wenye ‘vitambi’ ndiyo maana wameamua kukomalia mazoezi ili kujiweka sawa katika mwonekano.
Kwa upande wake, Jack aliwashauri warembo wengine kuvikimbia vyakula vinavyosababisha mwili ‘kuumuka’ na kupoteza mwonekano mzuri. 


Twitter Delicious Facebook Digg Favorites More