Katika kuonyesha amechoshwa na upweke, mwanamitindo Jokate Mwegelo
‘Kidoti’ ameibuka na kusema kuwa sasa anasaka mwanaume wa kumuoa huku
akitaja vigezo vya anayestahili kumuita mume.
Mwanamitindo Jokate Mwegelo ‘Kidoti’
Akizungumzia maisha yake ya kimapenzi, Jokate alisema kuwa hana ‘mtu’
ila atakapotokea mwenye vigezo anavyotaka, hatakuwa na sababu ya
kumkataa. “Kwa sasa sina mpenzi wala mchumba, akitokea sina kipingamizi
ila mbali na vigezo vingine awe na mapenzi ya dhati na mimi,” alisema
Jokate.
Jokate amekuwa msiri sana katika maisha
yake ya kimapenzi kiasi cha wengi kuamini ni msichana anayejiheshimu
sana ila aliwahi kuwa na uhusiano na mchezaji wa mpira wa kikapu,
Hasheem Thabeet anayekipiga kwenye Timu ya Oklahoma City Thunder ya
nchini Marekani.