'HAPPYBIRTHDAY’ YA HALIMA, BALAA....





Alichofanyiwa  Kimwana Manywele, Halima Haroun kwenye ‘bethidei’ yake kimetafsiriwa kuwa ni sawa na kumkufuru Mungu baada ya baadhi ya wageni waalikwa akiwemo Nasibu Abdul ‘Diamond’ kutumia juisi, maji na soda kumuogesha.

Ishu hiyo ilichukua nafasi ndani ya Hoteli ya Demage, Mwananyamala jijini Dar ambapo mwanadada huyo akiwalisha keki wageni waalikwa na baada ya zoezi hilo, watu walimvaa na kuanza kummiminia kichwani vinywaji hivyo na kumlowesha mwili mzima.
Kitendo hicho mbali na kulinogesha tukio hilo, wapo walio laani wakisema kuwa, tabia hiyo si nzuri kwani kutumia vinywaji kumuogesha mtu wakati kuna wanaovitafuta bila kuvipata ni sawa na kumkufuru Mungu.
“Dhambi iliyoje, watu wanatumia vinywaji kuogeshea mtu? Kuna faida gani sasa kufanya hivyo? Kama wana pesa zisizo na kazi ni bora wakawape masikini wanaoshinda na njaa kuliko kufanya vile?” alihoji Jumaa Shemputa wa Kinondoni jijini Dar.


Twitter Delicious Facebook Digg Favorites More