WOLPER: NIMEJIPANGA VILIVYO USIKU WA MATUMAINI 2014

MWANADADA anayefanya vizuri katika soko la filamu Bongo, Jacqueline Wolper amejitapa kuwa amejipanga vizuri katika kuhakikisha kuwa, siku ya tamasha kubwa la Usiku wa Matumaini atafanya mambo makubwa.

Mwanadada anayefanya vizuri katika soko la filamu Bongo, Jacqueline Wolper
Akipiga stori hivi karibuni, Wolper alisema anataka siku hiyo aweke historia katika ulimwengu wa ndondi hivyo anafanya mazoezi ya kufa mtu.
“Nipo katika maandalizi makubwa sana, sasa hivi naendelea na mazoezi ya kawaida wakati namsubiri mwalimu wangu ambaye naamini atanipa mbinu za kumkalisha chini mpinzani wangu,” alisema Wolper.


Twitter Delicious Facebook Digg Favorites More