NIKIKUTA MAKALIO HAYAPO, NAENDA KWA MCHUNGAJI


Aliyekua mtangazaji wa Runinga ya C2C ambaye kwa sasa ni mwigizaji, Lulu Semagongo ‘Anti Lulu’, ametoa kali baada ya kufunguka kuwa siku akiamka asubuhi na kukuta makalio yake hayapo, atakimbilia  kwa mchungaji akafanyiwe maombi.
Akizungumza na paparazi , mtangazaji huyo ambaye ana vituko lukuki, alisema kila siku anapoamka asubuhi, lazima aangalie kama makalio yake yapo ndiyo mambo mengine yafuatie.



“Jamani nikiamka kitandani, kabla ya kuoga na kupiga mswaki cha kwanza najitazama nyuma kama hili nililojaliwa na Mungu lipo na nisipolikuta, nakimbilia kwa mchungaji kuombewa fasta,” alisema Lulu.
Lulu aliongeza kuwa, hakuna kitu anachokipenda katika mwili kama makalio yake, hivyo hayupo tayari kuishi bila ya hayo makalio kwani ndiyo kila kitu katika mwili wake.
“Haya ndiyo kila kitu, usiniulize kwa nini nayapenda sababu naijua mimi mwenyewe,” alisema.



Twitter Delicious Facebook Digg Favorites More