Rais wa Madagascar awasili kuhudhuria mkutano wa SADC-TROIKA


 Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb.), (kushoto) akisalimiana na Mhe. Andry Rajoelina, Rais wa Madagascar mara baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam tarehe 11 Januari, 2013. Mhe. Rais Rajoelina yupo nchini  kwa ajili ya kuhudhuria Mkutano unaoendelea wa Asasi ya Siasa, Ulinzi na Usalama ya Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika (SADC-TROIKA).
 Mhe. Rais Rajoelina akiwa amefuatana na Mhe. Membe mara baada ya kupokelewa.
Mhe. Rais Rajoelina akisalimiana na Viongozi mbalimbali mara baada ya kuwasili.
 Mhe. Rais Rajoelina akipita katikati ya Gwaride  lililoandaliwa kwa heshima yake huku akisindikizwa na Mhe. Membe.
Mhe. Rais Rajoelina akiwa na Mhe. Membe wakifurahia burudani ya ngoma za utamaduni zilizokuwepo Uwanjani hapo mara baada ya kuwasili.


Twitter Delicious Facebook Digg Favorites More