DIDA: SIJAWAHI KUMTANDIKA VIBOKO MWANANGU

MAMBO Vipi mdau wangu, kama kawaida tunazidi kusonga mbele kwa kuwaletea mastaa ambao tayari Mungu amewajalia watoto. Kutokana na maombi ya wasomaji wengi wiki iliyopita kumtaka mtangazaji mahiri wa Kipindi cha Mitikisiko ya Pwani katika Redio ya Times Fm, Hadija Shaibu ‘Dida’, leo nimewaletea.
Hadi sasa Dida ana mtoto wa miaka nane aliyempatia jina zuri la Samira, mwenyewe anasema kuwa kwa mwanaye, mtu humuelezi kitu chochote. Twende katika mahojiano niliyofanya naye hapa chini:

SAUALA LA VIBOKO
“Unajua kama watoto jinsi walivyo siku zote ni watundu lakini suluhisho siyo adhabu ya kuwapiga,  mimi mara nyingi napenda sana kuzungumza na mwanangu pindi anapokosea na ni rahisi kunielewa maana mimi mwenyewe nikisikia hata mtoto wa jirani anapigwa, huwa naumia sana.”

ANAPENDA KUSAFIRI NAYE
“Katika safari zote ninazosafiri hasa za nje ya nchi, huwa sijisikii raha sana kama nikimuacha mwanangu. Mara nyingi nikiwa na muda mzuri huwa napenda kusafiri naye maana huko tunaweza kuongea naye mambo mbalimbali ya kumfunza kwa maana tunakuwa sehemu  yenye utulivu.”

MTOTO WAKE HAPENDI KUMUONA AMECHUKIA
“Kitu ambacho mwanangu hapendi kukiona kutoka kwangu ni mimi nikiwa nimekasirika, atajitahidi kwa hali na mali kunifanya nicheke au hata ajue ni sababu gani imenifanya
nikasirike.”

MWANAYE FULL VITUKO
“Kitu ambacho mtoto wangu ananipa raha ni pale anapokutana na mtu ambaye hamfahamu, kitu cha kwanza atamuuliza, unamjua Dida wa Mchomeeeee? Hahahaha!”

HAPENDI MWANAE AWE MTANGAZAJI
“Kwa kweli kuna msemo usemao maji hufuata mkondo lakini mimi sipendi mwanangu awe mtangazaji hususan taarab kwa sababu kuna mabifu mengi sana bora hata atangaze vipindi vingine aniache mimi mama yake nikomae nao.”


source:GP


Twitter Delicious Facebook Digg Favorites More