USHIRIKINA WAHUSISHWA UZAWA WA MTOTO WA AJABU.


 Mtoto wa ajabu aliyezaliwa na mwanamke Emeliana Wilson mkoani Mbeya hivi karibuni.

Mmoja wa watu waliyomuona mtoto huyo aliyezaliwa akiwa na macho yaliyoungana, kitu kama pembe katika paji la uso wake na kutokuwa na pua alisema yawezekana kuna mambo ya Kiswahili nyuma ya tukio hilo.
“Huyo mtoto siyo bure, yawezekana mama yake amekwenda kinyume na taratibu anazotakiwa kuzifuata mama mjamzito. Pia huenda kuna watu wabaya wameamua ‘kumchezea’ mama wa watu ili ajifungue mtoto wa ajabu kwa sababu wanazozijua wao,” alidai shuhuda huyo.


Mama wa mtoto huyo akizungumza na mwandishi wa habari wa gazeti moja litokalo kila siku alikiri kupata ujazito wa mtoto huyo baada ya kwenda kwa mganga wa jadi na kupewa dawa za miti shamba.
Aidha, mama huyo ameomba msaada kutoka kwa wasamaria wema wa kumuwezesha kumlea mwanaye kwa madai kwamba mumewe, Emmanuel Mbukwa ametoweka baada ya kumuona mtoto huyo wa ajabu. 


Twitter Delicious Facebook Digg Favorites More