Msanii wa filamu na
muziki Bongo , Zuwena Mohamed ‘Shilole’ amewaacha watu midomo wazi baada ya
kufanya kisomo na watoto yatima mchana na usiku akaangusha pati iliyokuwa na
matukio ya kumkufuru Mungu.
Matukio hayo yalijiri Desemba 18, mwaka huu ambapo Shilole alikuwa akisheherekea siku yake ya kuzaliwa bila kutaja umri.
Matukio hayo yalijiri Desemba 18, mwaka huu ambapo Shilole alikuwa akisheherekea siku yake ya kuzaliwa bila kutaja umri.
Majira ya mchana , dada
huyo alifanya kisomo nyumbani kwake Kinondoni, Dar pamoja na watoto yatima wa
Kituo cha Magomeni kisha akapata nao msosi na kuwapa msaada wa vyakula.
Wakati wa mchana, Shilole alionekana akiwa ndani ya mavazi nadhifu yaliyomsitiri vilivyo , akila pamoja na watoto hao na wageni wengine waalikwa wakiwemo wasanii wenzake.
Usiku wake baada ya matukio ya mchana, sherehe
ilihamia katika viwanja vya Leaders Club, Kinondoni ambapo kulikuwa na matukio kibao ya kumkufuru Mungu.